Saturday, July 11, 2015

TASWIRA ZA KIKAO CHA KAMATI KUU YA CCM MJINI DODOMA KILIVYOENDESHWA JANA

Mwenyekiti wa CCM Taifa na Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Jakaya Mrisho Kikwete (wa pili kushoto) akiongoza kikao cha Kamati Kuu Maalum cha CCM mjini
Dodoma, Kikao kilichochuja majina ya wagombea na kupata majina matano.
Katibu Mkuu wa CCM, Abdulrahman Kinana akitoa taarifa fupi ya wajumbe waliohudhuria kikao cha Kamati Kuu Maalum ambapo wajumbe 28 walihudhuria kati ya 32.
Wajumbe wa Kamati Kuu ya CCM wakipitia baadhi ya makabrasha wakati wa kikao cha Kamati Kuu Maalum.
Vijana wa CCM wakipakia mikoba yenye makabrasha ya Mkutano wa Halmashauri Kuu ya CCM Taifa 2015 ambao umeshaanza hivi punde katika ukumbi mpya wa Dodoma Convention Centre mjini Dodoma  uliozinduliwa juzi.