Tuesday, September 15, 2015

Picha ya Lowassa Yasababisha kifo


Mwalimu wa Shule ya Sekondari Manushi Kibosho, Wilaya ya Moshi Vijijini ameuawa saa chache baada ya ugomvi unaohusishwa na kuchanwa kwa picha ya mgombea urais wa Chadema, Edward Lowassa.

Mwalimu huyo, Demetus Dastan (33) maarufu kwa jina la Kidule, aliuawa Jumamosi iliyopita usiku na mwili wake kukutwa katika shamba la mtu aliyetajwa kuwa ni Joackim Massawe.

Kamanda wa Polisi Mkoa wa Kilimanjaro, Fulgence Ngonyani alisema kabla ya kuuawa, mwalimu huyo alikuwa amekwenda kunywa pombe katika klabu moja hapo kijijini. Inadaiwa kuwa akiwa klabuni, kulitokea ubishani kati yake na mtu mwingine uliotokana na kuchanwa kwa picha ya Lowassa ambao ulikwenda mbali na kusababisha wapigane.

Kamanda Ngonyani alisema waliamuliwa na wateja wengine waliokuwapo na baadaye mwalimu huyo aliondoka kurejea nyumbani na hakuonekana hadi mwili wake ulipookotwa.

Baadaye mwili wake ulikutwa shambani ukiwa na michubuko kidogo kwenye mguu wa kulia karibu na goti na shati lake likiwa limechanikachanika.

Polisi wamewakamata watu wawili akiwamo mmiliki wa klabu hiyo na mtu mwingine anayedaiwa kuwa aliongozana naye kurudi nyumbani huku mtu waliyepigana naye akiendelea kusakwa.

Rais Kikwete Amtaja Mhusika wa Sakata la Richmond....Asema ni Yule Anayetembea na Tundu Lissu Kila Siku Kwenye Kampeni


Rais Jakaya Kikwete amesema anashangazwa na Mwanasheria wa Chadema, Tundu Lissu kumtaka amtaje mhusika wa Richmond wakati mwenye Richmond yupo na anatembea naye mikoani.
 
Kikwete aliyasema hayo jana wakati akiwaaga wananchi wa Kigoma katika Uwanja wa Lake Tanganyika na kumtaka Lissu amtaje mwenye Richmond.
 
“Endapo Tundu Lissu atashindwa kumtaja mwenye Richmond, nitatoka hadharani na kumtaja mwenyewe,” alisema Kikwete.
 
Kabla ya mkutano huo, Rais Kikwete alifungua jengo la Mfuko wa Taifa wa Hifadhi ya Jamii, (NSSF) ambalo limejengwa kwa Sh7 bilioni.
 
Akifungua jengo hilo, aliwaomba wawekezaji na mifuko ya kijamii kuiga mfano wa NSSF kwa kuwekeza katika sekta ya majengo kwa kuwa yanapendezesha mji.
 
Kadhalika, Rais Kikwete alizindua jengo la Shirika la Nyumba la Taifa (NHC) pamoja na nyumba 36 za bei nafuu zilizopo katika eneo la Mlole, Kigoma Mjini.
 
Suala la Richmond imekuwa moja ya ajenda za CCM katika kampeni za urais hasa baada ya Waziri mkuu wa zamani Edward Lowassa aliyejiuzulu wadhifa huyo kwa kashfa hiyo kuhamia upinzani.
 
Kila sehemu ambako mgombea urais wa CCM anakwenda, suala hilo limekuwa likiibuliwa, huku Lowassa akisema yeye hakuhusika, bali alijiuzulu kuiokoa Serikali isianguke kwa kuwa ulikuwa uamuzi wa wakubwa.
 
Mgombea urais wa CCM, Dk John Magufuli amekuwa akienda mbali zaidi akisema akichaguliwa ataanzisha mahakama maalumu ya kushughulikia mafisadi wanaosababisha umaskini nchini.

Zitto Kabwe: CCM Imeoza.....Haiwezi Kubadilika Hata Akija MALAIKA Kuiongoza


KIONGOZI wa Chama cha ACT Wazalendo, Zitto Kabwe, amesema Chama Cha Mapinduzi (CCM) hata kipate malaika hakiwezi kubadilika, hivyo dawa pekee ni kukiondoa jumla madarakani.

Akizungumza juzi wakati wa mkutano wa kampeni uliofanyika katika kituo cha basi Tabata Segerea, Zitto alisema matatizo mengi ya nchi yamesababishwa na sera mbovu za CCM ambazo baadhi ya wagombea wake ndio waliokuwa wakizitunga, kuzitetea na kuzitekeleza.

“Kuna ambao wamekuwa watawala tangu tupate uhuru na bado wanataka waendelee kutawala, ukiwauliza wanasema tupeni tena kipindi kingine.