Saturday, June 21, 2014

ARGENTINA VS IRAN 1:0

Argentina yatinga raundi ya pili

Mfungaji bao la Argentina ,Lionel Messi
Lionel Messi alifunga bao la pekee na la ushindi katika dakika ya mwisho ya mechi baina ya Argentina na Iran ya kundi G.
Mechi hii ilikuwa na kila dalili ya kuishia sare tasa sawa na ile ya kwanza kati ya Iran na Nigeria ambapo vijana wa Carlos Queiroz walizima kila dalili ya shambulizi kutoka kwa Argentina.
Kocha wa Argentina Alejandro Sabella alimpiga pambaja Messi baada ya kipenga cha kukamilika kwa mechi hiyo kupulizwa .
Bao la Messi dhidi ya Iran.
Argentina walikuwa wameshinda mechi yao ya awali dhidi ya Bosnia Hercegovina.