Argentina yatinga raundi ya pili
Lionel Messi alifunga bao la pekee na la ushindi katika dakika ya mwisho ya mechi baina ya Argentina na Iran ya kundi G.
Mechi hii ilikuwa na kila dalili ya kuishia sare
tasa sawa na ile ya kwanza kati ya Iran na Nigeria ambapo vijana wa
Carlos Queiroz walizima kila dalili ya shambulizi kutoka kwa Argentina.